Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 9 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 144 2022-09-23

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DKT.OSCAR I. KIKOYO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa skimu za umwagiliaji Wilayani Muleba?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Oscar Ishengoma Kikoyo, Mbunge wa Muleba Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Kamati Shirikishi ya Umwagiliaji Mkoa na Ofisi ya Kilimo Wilaya ya Muleba imekamilisha tathmini ya kina ya mahitaji ya sasa ya skimu za umwagiliaji za Buyaga hekta 120, Kyamyorwa hekta 500, Kyota hekta 120 na Buhangaza hekta 600 na kupata gharama halisi za umaliziaji wa ujenzi wa skimu hizo. Serikali inaendelea na zoezi la kuainisha maeneo mengine yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji Wilayani Muleba likiwemo Bonde la Buligi lenye takribani hekta 5,000.

Mheshimiwa Spika, skimu hizo zitaingizwa katika mpango wa ujenzi na ukamilishaji wa skimu za umwagiliaji katika kipindi cha mwaka 2023/2024 na 2024/2025.