Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 1 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 19 2022-09-13

Name

Dr. Alfred James Kimea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA K.n.y. MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga bandari kavu eneo la Old Korogwe katika Halmashauri ya Mji Korogwe?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Alfred James Kimea, Mbunge wa Korogwe Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa bandari kavu hufanyika ili kuongeza ufanisi wa bandari zilizopo mwambao wa bahari na maziwa. Ujenzi wa bandari kavu huzingatia vigezo maalum ikiwa ni pamoja na kuondoa msongamano katika bandari iliyo karibu na bandari kavu na kusogeza huduma karibu na watumiaji wa mwisho. Aidha, kigezo kingine ni uwepo wa upembuzi yakinifu unaobainisha mahitaji ya bandari kavu husika ili kuwa na msingi wa kufanya maamuzi sahihi.

Mheshimiwa Spika, kutokana na maelezo hayo, eneo la Old Korogwe halijabainishwa kwa sasa kwamba linafaa kujengwa bandari kavu. Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari itafanya tathmini kuona umuhimu wa uwepo wa bandari kavu katika eneo la Old Korogwe. Ahsante.