Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 8 2022-09-13

Name

Bahati Keneth Ndingo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. BAHATI K. NDINGO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaweka mfumo utakaoruhusu wafungwa kupata haki ya faragha na wenza wao?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bahati Keneth Ndingo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutoa haki mbalimbali kwa wafungwa walioko magerezani kwa mujibu wa sheria. Haki ya faragha kwa wafungwa na wenza wao itaanza kutolewa pale ambapo mifumo ya kisheria, na miundo mbinu ya magereza itakapokidhi kutolewa kwa haki hiyo. Masuala mengine yatakayozingatiwa ni usalama, mila na desturi za Watanzania, kwani haki hiyo inatakiwa kutekelezwa kwa faragha.