Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 1 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 5 2022-09-13

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE K.n.y. MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: -

Je, ni fedha kiasi gani zimerudishwa kwa wadai wa VAT wanaoidai Serikali kuishia mwaka wa fedha 2021/2022?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deodatus Philip Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mwaka 2021/2022, jumla ya Shilingi bilioni 916.68 zililipwa kwa wadai wa VAT, sawa na ufanisi wa asilimia 431.7 ikilinganishwa na bajeti iliyotengwa. Ufanisi huu umetokana na hatua iliyochukuliwa na Serikali ya kuhakiki maombi ya wadai kwa kuzingatia viashiria hatarishi badala ya utaratibu wa awali wa kuhakiki maombi yote kwa asilimia 100.

Mheshimiwa Spika, utaratibu huo umeongeza kasi ya uhakiki na ulipaji wa madai ya marejesho ya VAT na kupunguza ucheleweshwaji kwa kuwa uhakiki unafanyika kwa wakati. Hatua na mafanikio hayo yanalenga kuchochea ukuaji wa uchumi, uwekezaji na kulinda mitaji ya wawekezaji na wafanyabiashara hapa nchini. Ahsante.