Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 14 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 171 2022-02-18

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kiwanja cha Michezo katika Wilaya ya Hai?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saasisha Elinikyo Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sera ya Maendeleo ya Michezo ya mwaka 1995, Ibara ya 7 (i) hadi (vii) imetoa maelekezo juu ya ujenzi na utunzaji wa viwanja vya michezo. Sera imezielekeza Halmashauri kutenga maeneo ya viwanja kila wanapopima makazi ya watu na pia kutumia wadau mbalimbali na raslimali zilizopo katika Halmashauri zao ili kuwajengea wananchi viwanja ili wapate mahali sahihi pa kushiriki shughuli za michezo ili kukuza na kulinda afya zao na pia kupata eneo la kutolea burudani za wazi.

Mheshimiwa Spika, kutokana na Mkakati wa Taifa wa utekelezaji wa Sera ya Maendeleo ya Michezo wa mwaka 2022 mpaka 2032, nitumie nafasi hii kutoa rai kwa uongozi wa Halmashauri ya Hai na Halmashauri zote nchini pamoja nanyi Waheshimiwa Wabunge wote kuendelea kutenga fedha za ujenzi wa viwanja katika viwanja katika bajeti zetu za Halmashauri husika na kuendelea kuwashirikisha wadau mbalimbali wa michezo katika kukamilisha azma hiyo ya kuwa na viwanja na miundombinu bora ya michezo mbalimbali hapa nchini. Ahsante. (Makofi)