Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 13 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 155 2022-02-17

Name

Amour Khamis Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbe

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: -

Je, Serikali inakusanyaje ushuru kwenye Boti zinazoondoka saa moja kamili asubuhi katika Bandari ya Dar es Salaam ilhali watumishi hufika kazini kuanzia saa moja na nusu na zaidi?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Amour Khamis Mbarouk, Mbunge wa Tumbe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), pamoja na wadau wote muhimu ikiwemo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), hutoa huduma za kibandari kwa saa 24 kwa siku saba za juma katika Jiji la Dar es Salaam.

Mheshimiwa Spika, Kanuni za Utumishi kwa Wafanyakazi wa Bandari za mwaka 2019 zimetoa Mwongozo wa Muda wa Kuwa Kazini, ambapo wafanyakazi wote wa Bandari wanaopangiwa maeneo ya kutoa huduma kwa meli ama boti za mizigo hupaswa kuingia kazini kwa zamu (shifts) tatu kama ifuatavyo; saa 1:00 asubuhi hadi saa 9:00 alasiri; shift ya kwanza; saa 9:00 alasiri hadi saa 5:00 Usiku; shift ya pili na saa 5:00 Usiku hadi saa 1:00 asubuhi shift ya tatu.

Mheshimiwa Spika, aidha, watumishi wa TPA wanaopangiwa zamu katika eneo la boti zinazosafiri kati ya Dar es Salaam na Zanzibar wanapaswa kuwepo kwenye eneo la kazi na kuhakikisha kuwa huduma zote muhimu za kibandari zinatolewa ikiwemo ukusanyaji wa mapato ya Bandari. Nitumie fursa hii kuitaka TPA kusimamia kwa karibu utaratibu uliowekwa. Ahsante. (Makofi)