Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 12 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 145 2022-02-16

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Handeni – Kiberashi – Kiteto – Chemba hadi Singida utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi wa ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Omari Mohamed Kigua, Mbunge wa Kilindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Handeni – Kibirashi – Kijungu – Kibaya – Njoro – Olboloti – Mrijo Chini – Dalai – Bicha – Chambalo - Chemba – Kwa Mtoro hadi Singida ni barabara ya mkoa yenye urefu wa kilometa 461 inayounganisha Mikoa ya Tanga, Dodoma, Manyara na Singida. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya ujenzi wa barabara hii umeanza ambapo upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami ulikamilika mwaka 2018. Zabuni ya kazi ya ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya Handeni – Mufulate (Kilometa 20) zilishatangazwa na Mkandarasi kupatikana. Rasimu ya Mkataba imepelekwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kupata idhini (vetting) ya kusaini Mkataba.

Mheshimiwa Naibu Spika, maandalizi ya kutangaza zabuni ya ujenzi kwa sehemu ya kutoka Mafuleta – Kwediboma yenye urefu wa kilometa 30 yanaendelea na zabuni itakuwa imetangazwa kabla ya Juni, 2022. Aidha, Serikali itaendelea na ujenzi wa barabara hii kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante. (Makofi)