Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 12 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 144 2022-02-16

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya Lushoto – Magamba – Lukozi – Mlalo hadi Umba Junction kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Husna Juma Sekiboko, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Lushoto – Magamba – Lukozi – Mlalo hadi Umba Junction ni barabara ya Mkoa yenye urefu wa kilometa 66.23 na inasimamiwa na Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS), Mkoa wa Tanga.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikitekeleza ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami kwa awamu kutegemeana na upatikanaji wa fedha. Hadi sasa jumla ya kilometa 9.1 kati ya Lushoto na Mazinde Juu zimejengwa kwa kiwango cha lami. Mwaka huu wa fedha 2021/2022, jumla ya Shilingi milioni 420 zimetengwa ili kuendeleza ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami kwa kipande chenye urefu wa mita 400. Kazi za ujenzi zilianza mwezi Januari, 2022 na kazi zinategemewa kukamilika mwezi Juni, 2022. Hadi tarehe 10 Februari, 2022 kazi zilikuwa zimefikia asilimia 15.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea na ujenzi wa barabara hii kwa awamu kulingana na upatikana wa Fedha. Ahsante.