Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 12 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 135 2022-02-16

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kuigawa Wilaya ya Kilolo kuwa na Halmashauri mbili?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Justin Lazaro Nyamoga, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mchakato wa kuanzisha eneo la utawala la wilaya unafanyika kwa Mujibu wa Sheria, Kanuni na kwa kuzingatia mwongozo wa kuanzishwa maeneo mapya ya utawala wa mwaka 2014. Aidha, maombi ya kuanzisha wilaya mpya yanatakiwa kujadiliwa na kupitishwa kwenye Vikao vya Kisheria ngazi ya Vijiji, Kata, Baraza la Madiwani, Kamati ya Ushauri ya Wilaya na Kamati ya Ushauri ya Mkoa. Maombi hayo yanawasilishwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa ajili ya uchambuzi na uhakiki na baadaye kuishauri mamlaka ipasavyo juu ya suala hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Iringa haujawasilisha mapendekezo yanayohusu kugawa Wilaya ya Kilolo ili kuwe na Halmashauri mbili. Napenda kumshauri Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Kilolo kufuata utaratibu uliolekezwa hapo juu, ahsante.