Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 11 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 128 2022-02-15

Name

Santiel Eric Kirumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaboresha Bandari Kavu ya Isaka?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Santiel Eric Kirumba, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania kwa maana ya TPA, imenunua na kupeleka vifaa vya kuhudumia mizigo ambavyo ni forklift moja na reach stacker moja ambavyo vinatumiwa na Shirika la Reli Tanzania kwa maana TRC kuendesha Bandari Kavu ya Isaka, Shinyanga kwa sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo la kununua na kupeleka vifaa hivyo katika Bandari Kavu ya Isaka ni kuongeza ufanisi wa utoaji huduma za usafirishaji mizigo kati ya Dar es Salaam, mikoa ya Jirani na Shinyanga na Nchi jirani za Rwanda, Congo na Burundi. Bandari Kavu ya Isaka imekuwa ikitumika japo kwa kiwango kidogo kutokana na changamoto ya mabehewa ya kubeba makasha na injini inayoikabili. TRC mwaka jana Disemba, 2021, imepokea mabehewa 44 na injini tatu za treni kwa ajili ya kuhudumia mizigo kati ya Bandari ya Dar es Salaam na Bandari Kavu ya Isaka. Aidha, Serikali kupitia TPA na TRC inaendelea kufanya ushawishi kwa wateja wa bandari na wasafirishaji wakiwemo wale wa kutoka Nchi jirani za Rwanda, Congo na Burundi kutumia zaidi Bandari Kavu ya Isaka. Ahsante. (Makofi)