Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 11 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 121 2022-02-15

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU K.n.y. MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka Boti ya kubebea Wagonjwa katika vijiji zaidi ya saba vilivyopo Mwambao mwa Ziwa Tanganyika katika Jimbo la Nkasi Kusini ambavyo havina huduma ya Zahanati wala Kituo cha Afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vicent Paul Mbogo, Mbunge wa Jimbo la Nkasi Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti; Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022 imetenga shilingi bilioni 35.1 kwa ajili ya ununuzi wa magari ya wagonjwa 195 ambayo yatapelekwa kwenye Halmashauri zote nchini ikiwemo Halmashauri ya Nkasi Kusini. Aidha, Serikali imekwishapeleka fedha shilingi milioni 250 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya King’ombe kwenye Kata ya Kala ambapo ujenzi unaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya Nkasi imetenga shilingi milioni 23 kwa ajili ya kufanya matengenezo ya magari ya kubebea wagonjwa na Boti zinazotoa huduma ili kuboresha na kuimarisha huduma kwa wagonjwa. Ahsante.