Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 19 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 159 2016-05-13

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANTONY C. KOMU (K.n.y. MHE. HAWA S. MWAIFUNGA) aliuliza:-
Kumekuwa na ukiukwaji mkubwa wa maadili ya utumishi ndani ya Jeshi la Polisi kutokana na hilo Askari wengi wanaonekana kukosa weledi kwa kujihusisha na matendo yanayokinzana na maadili ya utumishi wa umma:-
(a) Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha kuwa Askari wasio na sifa wanachukuliwa hatua?
(b) Je, zoezi la kuhakiki vyeti vya Askari wasio na sifa ndani ya Jeshi la Polisi limefikia wapi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Subira Mwaifunga, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Polisi lina utaratibu wa kuwachukulia hatua za kisheria askari wachache ambao wanachafua taswira na kazi nzuri inayoendelea kufanywa na Jeshi la Polisi kwa kukiuka sheria, kanuni na taratibu pamoja na kujihusisha na vitendo vinavyokinzana na maadili ya utumishi wa umma. Aidha, tumeamua kusitisha kwa muda ajira zote kwenye vyombo vyote vilivyomo ndani ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi likiwemo Jeshi la Polisi na kupitia utaratibu wa kutoa ajira ili kuondoa uwezekano wa watu wasio na sifa kujipenyeza na kupata ajira ndani ya vyombo vilivyo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, zoezi la uhakiki wa vyeti vya askari wasio na sifa ndani ya Jeshi la Polisi linaendelea. Mpaka sasa jumla ya askari 19 wamechukuliwa hatua mbalimbali za kisheria.