Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 9 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 102 2022-02-11

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga mnara wa mawasiliano ya simu katika Kata ya Mtego wa Noti ili wananchi waweze kupata huduma ya mawasiliano ya simu?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nashon William Bidyanguze, Mbunge wa Kigoma Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) ilifanya tathmini ya upatikanaji wa huduma za mawasiliano kwa kutembelea Kata ya Mtego wa Noti mnamo tarehe 19 Disemba, 2021 na kubaini kuwa kuna changamoto ya upatikanaji wa huduma za mawasiliano katika Kata hiyo.

Mheshimiwa Spika, Kata ya Mtego wa Noti imeainishwa ili kuingizwa katika zabuni ijayo ya kufikisha huduma za mawasiliano ya simu inayotarajiwa kutangazwa katika mwaka huu wa fedha 2021/2022. Aidha, ujenzi wa mnara huo utaanza mara baada ya kupatikana mtoa huduma na hivyo wananchi wa kata hiyo watarajie kupata huduma za mawasiliano ya simu mara baada ya kukamilika ujenzi huo, ahsante.