Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 9 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 99 2022-02-11

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza: -

Je, kwa nini Serikali isiweke utaratibu wa mafunzo ambao utahakikisha wanafunzi wa vyuo vikuu wanapangiwa moja kwa moja maeneo ya kwenda kujifunza badala ya utaratibu wa sasa wa mwanafunzi kutafuta mwenyewe?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Asha Abdullah Juma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mitaala ya vyuo vikuu huwataka wanafunzi kukamilisha masomo kwa kufanya mafunzo kwa vitendo katika taasisi mbalimbali za Serikali na binafsi. Utaratibu uliopo ni kwamba vyuo vikuu vinaainisha maeneo wanayokusudia kupeleka wanafunzi na kuomba nafasi za kufanyia mazoezi kwa vitendo. Baada ya maeneo ya kufanya mazoezi kwa vitendo kupatikana, vyuo huwapatia wanafunzi barua za kuwatambulisha kwenye taasisi husika ili waweze kupokelewa.

Mheshimiwa Spika, wanafunzi wana uhuru pia wa kutafuta maeneo ya kufanyia mafunzo kwa vitendo na kukijulisha chuo kwa taarifa rasmi. Baada ya wanafunzi kupata nafasi katika Taasisi husika vyuo huwapa barua za utambulisho ili waweze kupokelewa na kuendelea kufanya mafunzo kwa vitendo.

Mheshimiwa Spika, napenda kutoa wito kwa vyuo vikuu nchini kudumisha mahusiano na taasisi mbalimbali vikiwemo viwanda na kuwa na mikataba ya makubaliano ya kupeleka na kupokea wanafunzi kwenye mafunzo kwa vitendo. Nakushukuru. (Makofi)