Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 8 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 91 2022-02-10

Name

Najma Murtaza Giga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza: -

Je, Serikali haioni umuhimu wa kurudisha masomo ya ziada ya kazi za mikono kama vile useremala, upishi, ushonaji, kilimo na ujenzi katika shule za msingi na sekondari ili kupunguza changamoto ya ajira?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Najma Murtaza Giga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kufundisha masomo ya kazi za mikono kama vile Useremala, Upishi, Ushonaji, Kilimo na Ujenzi ili kuwajengea wanafunzi stadi mbalimbali za maisha zitakazowasaidia kukabiliana na changamoto ya upatikanaji wa ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutilia mkazo masomo ya ziada ya kazi za mikono katika ngazi mbalimbali za elimu. Kwa mfano, katika ngazi ya Elimu ya Msingi, Stadi za Useremala, Upishi, Ushonaji, Kilimo na Ujenzi hufundishwa katika somo la Stadi za Kazi kuanzia Darasa la Tano. Pia, masomo ya ziada ya kazi za mikono yamekuwa yakifundishwa kama masuala mtambuka kupitia vilabu vya masomo. Katika ngazi ya sekondari, stadi na maarifa haya hufundishwa katika somo la Home Economics pamoja na masomo ya ufundi yakiwemo ya useremala na ujenzi. Vilevile, somo la Kilimo hufundishwa ngazi ya sekondari. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali inaendelea na mapitio ya mitaala ya elimu na mafunzo katika ngazi mbalimbali kwa lengo la kuboresha elimu na mafunzo yatolewayo ili yaweze kutoa stadi mbalimbali na kukidhi mahitaji ya jamii kwa maendeleo ya Taifa letu. Hivyo, nawaomba wadau mbalimbali wa elimu kuendelea kushiriki kikamilifu katika mchakato huu kwa kutoa maoni na ushauri utakaosaidia kuboresha elimu yetu. Nakushukuru. (Makofi)