Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 8 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 85 2022-02-10

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itafikisha umeme kwenye vijiji ambavyo bado havijafikiwa Wilayani Chunya pamoja na Makao Makuu ya Kata za Nkung’ungu, Lualaje, Mafyeko na Kambikatoto?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Masache Njelu Kasaka, Mbunge wa Lupa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu – Mzunguko wa Pili unaolenga kufikisha miundombinu ya umeme katika vijiji vyote ambavyo vilikuwa havijafikiwa na huduma ya umeme Tanzania Bara.

Mheshimiwa Spika, Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa niaba ya Serikali umeingia mkataba na Kampuni ya M/S Electrical Transmission and Distribution Construction and Maintenance Company Limited kutekeleza mradi huu katika Mkoa wa Mbeya ambao utekelezaji wake umekwishaanza kwa Mkandarasi kukamilisha uhakiki na kuagiza vifaa vitakavyotumika katika ujenzi.

Mheshimiwa Spika, mradi wa kupeleka umeme katika Wilaya ya Chunya unahusisha ujenzi wa njia ya umeme ya msongo kilovoti 33 zenye urefu wa kilomita 245.5; kilomita 12 ya njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 0.4; ufungwaji transfoma 12 za KVA 50; pamoja na kuunganisha wateja wa awali 814. Gharama ya mradi ni Shilingi bilioni 10.656 na utekelezaji wa mradi huu unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2022.