Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 8 Water and Irrigation Wizara ya Maji 84 2022-02-10

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: -

Je, ni lini ahadi iliyotolewa wakati wa kampeni za Urais ya ujenzi wa mabwawa mawili ya maji katika Wilaya ya Kiteto itatekelezwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Edward Kisau Olelekaita, Mbunge wa Jimbo la Kiteto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hali ya upatikanaji wa huduma ya majisafi na salama katika Wilaya ya Kiteto kwa sasa ni asilimia
52.58. Katika kuboresha huduma ya majisafi na salama katika Wilaya ya Kiteto, Serikali katika mwaka fedha 2021/2022, inatekeleza miradi katika Vijiji 21 vya Nchinila, Engusero, Ngipa, Nasetani, Ngarenaro, Mafichoni, Kibaya Kati, Kanisani Bomani, Magubike na Msakasaka. Vijiji vingine ni Jangwani, Magungu, Kaloleni, Majengo Mapya, Msikitini, Vumilia, Esuguta na Kiperesa.

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa miradi hiyo unahusisha ujenzi wa matangi 11 yenye jumla ya ujazo wa lita 1,325,000, ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 99.49 na ujenzi wa vituo 69 vya kuchotea maji. Utekelezaji wa miradi hiyo umefikia wastani wa asilimia 10 na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni, 2022.

Mheshimiwa Spika, Mpango wa muda mrefu, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022, imefanya mapitio ya usanifu wa Bwawa la Maji la Dongo na usanifu wa ukarabati wa Mabwawa ya Dosidosi na Kijungu na taratibu za kupata wakandarasi zitakamilika kabla ya mwezi Juni, 2022. Ujenzi wa Bwawa la Dongo pamoja na ukarabati wa Mabwawa ya Dosidosi na Kijungu unatarajiwa kuanza katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023.