Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 7 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 75 2022-02-09

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami kwa barabara ya Mwanangwa – Misasi – Kahama?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Alexander Pastory Mnyeti, Mbunge wa Misungwi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Mwanangwa – Misasi – Kawekamo – Solwa – Kahama yenye urefu wa kilometa 150, ilifanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na kukamilika mwaka 2017 kwa gharama ya shilingi milioni 798.8. Kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, wakati Serikali ikiendelea na juhudi za kutafuta fedha za ujenzi kwa kiwango cha lami, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara (TANROADS), inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali ya barabara hii ili iendelee kupitika kipindi chote cha mwaka. Katika mwaka wa fedha 2021/2022, jumla ya shilingi milioni 2,809.304 zimetengwa kwa matengenezo mbalimbali pamoja na ujenzi wa madaraja saba katika maeneo yanayoathiriwa na mafuriko. Madaraja hayo ni madaraja mawili katika eneo la Mwanzugi, madaraja matatu katika eneo la Mwakitolyo na madaraja mawili katika eneo la Solwa.

Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imekamilisha ujenzi wa kilometa 5.15 kwa kiwango cha lami katika eneo la Kahama kuelekea Solwa. Ahsante.