Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 7 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 72 2022-02-09

Name

Katani Ahmadi Katani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tandahimba

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE K.n.y. MHE. KATANI A. KATANI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawalipa wakulima wa Korosho fedha zao walizofanya biashara msimu wa 2017/2018 na iliyokuwa Benki ya Covenant iliyofungwa kabla ya wakulima hawajatoa fedha zao?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Katani Ahmed Katani, Mbunge wa Tandahimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Benki Kuu ya Tanzania iliifutia leseni iliyokuwa Benki ya Covenant mnamo tarehe 4 Januari, 2018 kwa mujibu wa Sheria ya Mabenki na Taasisi za Kifedha ya mwaka 2006.

Mheshimiwa Spika, baada ya kuifutia leseni, Benki Kuu iliiteua Bodi ya Bima ya Amana (DIB) kuwa mfilisi wa Benki hiyo kwa mujibu wa sheria. Kuanzia mwezi Machi, 2018, Bodi ya Bima ya Amana ilianza zoezi la kulipa fidia ya Bima ya Amana ya kiasi kisichozidi shilingi 1,500,000 kwa wateja waliostahili kulipwa Bima ya Amana wakiwemo wakulima wa korosho wa Wilaya ya Tandahimba na zoezi hilo bado linaendelea kwa wateja ambao hawajajitokeza kuchukua fidia hiyo.

Mheshimiwa Spika, hadi kufikia mwezi Desemba, 2021, jumla ya shilingi 332,715,894.00 zililipwa kwa wakulima wa korosho 1,078 kati ya wakulima 1,346 wa Wilaya ya Tandahimba waliokuwa na amana katika Benki ya Covenant. Kiasi hicho ni sawa na asilimia 98 ya kiasi cha shilingi 337,992,095.00 zilizotengwa kwa ajili ya kulipa fidia katika Kituo cha Tandahimba.

Mheshimiwa Spika, aidha, Bodi ya Bima ya Amana inaendelea na zoezi la ufilisi wa Benki hiyo kwa kukusanya mali na madeni ya Benki hiyo ili kupata fedha za kuwalipa wateja waliokuwa na amana zinazozidi shilingi 1,500,000 ambapo kwa mujibu wa sheria na taratibu za ufilisi kiasi kitakacholipwa kitategemea fedha zitakazopatikana kutokana na kuuza mali za Benki hiyo. Ahsante.