Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 6 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 66 2022-02-08

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Vyuo Vikuu katika Mkoa wa Songwe?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Neema Gerald Mwandabila, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali huanzisha Vyuo Vikuu na kutoa vibali kwa watu na taasisi binafsi kuanzisha Vyuo Vikuu kwa lengo la kuwawezesha Watanzania wengi zaidi kupata fursa ya kusoma Elimu ya Juu. Vyuo Vikuu vilivyopo hupokea wanafunzi kutoka Mikoa yote ya Tanzania Bara, Visiwani pamoja na wanafunzi kutoka nje ya nchi. Huo ndiyo utamaduni wa Vyuo Vikuu duniani kote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mkoa wa Songwe kuna Kituo cha Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) kilichopo katika Makao Makuu ya Mkoa wa Songwe. Pia, kuna Kampasi ya Myunga ambayo ni Tawi la Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) iliyopo katika Wilaya ya Momba. Hivyo, wananchi wanashauriwa kuendelea kuvitumia Vyuo hivyo na vingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Serikali inaendelea na mpango wa kuboresha Vyuo Vikuu na Taasisi za Elimu ya Juu zilizopo kwa kukarabati na kujenga miundombinu mipya pamoja na kuongeza vifaa vya kisasa vya kufundishia na kujifunzia kwa lengo la kuongeza nafasi za udahili na ubora wa Elimu ili kukidhi mahitaji Kitaifa, Kikanda na Kimataifa. Nakushukuru. (Makofi)