Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 6 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 63 2022-02-08

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENARDETA K. MUSHASHU aliuliza: -

Je, ni lini wananchi waliokuwa wameweka fedha zao katika Benki ya Wakulima wa Kagera ya KFCB iliyofungwa na Benki Kuu Mwaka 2018 watarejeshewa fedha zao?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Benardeta Kasabago Mushashu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mnamo tarehe 4 Januari, 2018, Benki Kuu ya Tanzania iliifutia leseni ya kufanya biashara, Benki ya Wakulima wa Mkoa wa Kagera (Kagera Farmers’ Cooperative Bank Limited) kwa mujibu wa Sheria ya Mabenki na Taasisi za Fedha ya mwaka, 2006.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuifutia leseni benki hiyo, Benki Kuu ya Tanzania iliiteua Bodi ya Bima ya Amana (Deposit Insurance Board – DIB) kuwa mfilisi wa Benki hiyo kwa mujibu wa sheria. Ambapo kuanzia mwezi Machi, 2018 ilianza zoezi la kulipa fidia ya Bima ya Amana ya kiasi cha hadi shilingi 1,500,000 (Pay-out of insured deposits), kwa wateja waliostahili kulipwa Bima ya Amana. Zoezi hilo bado linaendelea kwa wateja ambao hawajajitokeza kuchukua fidia hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sanjari na zoezi hilo la kulipa fidia kwa wateja ambao hawajajitokeza, Bodi ya Bima ya Amana inaendelea na zoezi la ufilisi wa Benki hiyo kwa kukusanya mali na madeni ya Benki hiyo ili kupata fedha za kuwalipa wateja waliokuwa na amana zao katika benki hiyo, isiyozidi shilingi 1,500,000/=, ambapo kwa mujibu wa sheria na taratibu za ufilisi kiasi kitakacholipwa kitategemea, fedha zilizopatikana kutokana na kuuza mali za benki hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Disemba, 2021 jumla ya Sh.737,137,082.44 zimeshalipwa kwa wateja 1,389 waliokuwa na amana kwenye Benki ya Wakulima wa Mkoa wa Kagera - KFCB kati ya wateja 7,096 wanaostahiki kulipwa fidia hiyo. Malipo hayo ni sawa na asilimia 90.25 ya kiasi cha Sh.816,801,700.15 zilizotengwa kwa ajili ya kulipa fidia. Ahsante.