Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 6 Investment and Empowerment Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji 62 2022-02-08

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Viwanda vya Kusindika Maziwa katika Mkoa wa Arusha?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zaytun Seif Swai, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Arusha ni moja ya mikoa yenye uzalishaji mkubwa wa maziwa ambapo unazalisha takriban lita 30,550,500 kwa mwaka. Mkoa wa Arusha una jumla ya viwanda 18 viwanda ambavyo ni vikubwa na vidogo vya kusindika maziwa vilivyosajiliwa na Bodi ya Maziwa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uwezo uliosimikwa wa kusindika maziwa kwa viwanda tajwa ni kiasi cha takriban lita 43,789,200 kwa mwaka. Lakini hata hivyo, usindikaji halisi ni lita 6,315,400 kwa mwaka. Maziwa mengi hayaingii kwenye soko rasmi na kushindwa kupelekwa viwandani kwa ajili ya kuchakatwa, kutokana na ukusanyaji mdogo wa maziwa yanayozalishwa na wafugaji katika maeneo hayo. Jambo linaloathiriwa na ukosefu wa mifumo mizuri ya ukusanyaji wa maziwa (collection centres).

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati wa Serikali ni kushirikiana na sekta binafsi kuendelea kuhamasisha ujenzi wa miundombinu ya kukusanyia maziwa ili viwanda vyote vipate maziwa ya kutosha katika mkoa wa Arusha na mikoa mingine nchini, yenye uzalishaji mkubwa wa maziwa. Hii itasaidia kuongeza tija kwenye mnyororo wa thamani wa maziwa nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.