Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 6 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 58 2022-02-08

Name

Rashid Abdalla Rashid

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiwani

Primary Question

MHE. MARIAM AZZAN MWINYI K.n.y. MHE. RASHID ABDALLA RASHID aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga tuta la kuzuia maji ya Bahari yanayoharibu mashamba ya Wananchi wa Vijiji vya Nanguli, Jundamiti, Mwambe na Kiwani katika Jimbo la Kiwani?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdalla Rashid, Mbunge wa Kiwani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mabadiliko ya tabianchi kote duniani kwa sasa yapo dhahiri na athari zake zinaendelea kuonekana hapa nchini. Mojawapo ya athari hizo ni kuongezeka kwa kina cha bahari katika maeneo mbalimbali ya fukwe likiwemo Jimbo la Kiwani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na changamoto hiyo, Serikali imeanza kufanya upembuzi wa awali kwenye fukwe zilizoathiriwa nchini kutokana na kujaa maji ya bahari ili hatimaye kujenga kingo za kuzuia maji ya bahari kuingia kwenye makazi na mashamba ya wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza juhudi za wananchi na Mfuko wa TASAF katika Jimbo la Kiwani kwa kuanza kushughulikia changamoto hizi na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Jimbo la Kiwani ni miongoni mwa maeneo yatakayofanyiwa upembuzi yakinifu ili kubaini hatua zinazopaswa kuchukuliwa baadaye. Ahsante.