Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 57 2022-02-08

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: -

Je, Serikali haioni kuwa kuajiri Walimu bila kujali muda wa kuhitimu, baadaye baadhi yao watashindwa kuajiriwa kutokana na umri wao kuwa mkubwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Conchesta Leonce Rwamlaza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika mwaka wa fedha 2020/2021 iliajiri Walimu wa shule za msingi na sekondari wapatao 6,949.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuhakikisha haki inatendeka katika ajira hizo, Serikali ilitumia mfumo wa kielektroniki (Online Teachers’ Employment Application System – OTEAS) kwa ajili ya kupokea, kuchakata na kuwapangia vituo kwa mujibu wa vigezo vilivyowekwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya vipaumbele vya ajira hizo ni cha wahitimu waliohitimu miaka ya nyuma zaidi. Katika ajira hizo takribani asilimia 75.6 ni wahitimu kati ya mwaka 2014 hadi 2017 na wachache, takribani asilimia 24.4, ni wahitimu waliohitimu kati ya mwaka 2018 hadi 2019 ambao wengi walikuwa na mahitaji maalum.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuajiri Walimu kwa kuzingatia mwaka wa kuhitimu ambapo waliohitimu muda mrefu watapewa kipaumbele. Ahsante.