Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 56 2022-02-08

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatoa vifaa tiba na dawa za kutosha kwenye vituo vya afya na zahanati zote katika Halmashauri ya Wilaya ya Msalala?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi, Mbunge wa Jimbo la Msalala, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuboresha upatikanaji wa dawa na vifaatiba, katika Mwaka wa Fedha 2021/2022, Serikali ilitenga shilingi bilioni 11.3 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa na vifaatiba ambapo Halmashauri ya Msalala imetengewa shilingi milioni 376 kati ya fedha hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Msalala katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2021/2022, imetenga bajeti ya dawa na vifaatiba kiasi cha shilingi bilioni 1.5 ambapo hadi kufikia Desemba, 2021 kiasi cha shilingi milioni 403.2, sawa na asilimia 38.1 kimetolewa.

Aidha, Kituo cha Afya Isaka na Mwalugulu vimetengewa vifaa vya jumla ya shilingi milioni 600 na Zahanati za Matinje, Mwakima na Kabondo zimetengewa jumla ya shilingi milioni 150 kwa ajili ya vifaa na vifaatiba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na Serikali Kuu, halmashauri zimeelekezwa kuimarisha na kudhibiti makusanyo ya fedha za uchangiaji wa huduma za afya ili kuhakikisha vifaatiba na dawa vinapatikana ipasavyo. Ahsante.