Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 55 2022-02-08

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: -

Je ni lini Serikali itapeleka Watumishi wa kada ya Ualimu na Afya katika Wilaya ya Lushoto?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Lushoto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua mahitaji ya walimu na watumishi wa kada ya afya nchini kote ikiwemo Wilaya ya Lushoto. Wilaya ya Lushoto ina upungufu wa walimu kwa asilimia 44.4 na watumishi wa kada ya afya kwa asilimia 66.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2020/2021 Serikali iliajiri watumishi 9,675 katika kada za afya na uwalimu ambapo Wilaya ya Lushoto ilipelekewa walimu 86 na watumishi wa kada ya afya 10.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zoezi la ajira ni endelevu na Halmashauri ya Lushoto itapewa kipaumbele. Ahsante.