Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 5 Water and Irrigation Wizara ya Maji 51 2022-02-07

Name

Robert Chacha Maboto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda Mjini

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE K.n.y. MHE. ROBERT C. MABOTO Aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itasambaza maji katika mitaa ya pembezoni kwa Kata za Kabasa, Guta, Kuzungu, Sazira, Nyatwali, Mcharo na Wariku katika Mji wa Bunda?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI Alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Robert Chacha Maboto, Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, jukumu la Serikali ni kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya majisafi na salama na endelevu. Hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Wilaya ya Bunda ni wastani wa asilimia 69.

Mheshimiwa Spika, Kata ya Guta inapata huduma ya majisafi na salama kupitia mtandao wa maji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Bunda. Aidha, kwa Kata za Kabasa, Sazira, Mcharo, Kunzugu, Wariku na Nyatwali zinapata huduma ya maji kupitia visima thelathini (30) vilivyofungwa pampu za mikono.

Mheshimiwa Spika, katika kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji kwenye kata hizo, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022, inatekeleza ujenzi wa miradi ya maji katika Kata za Nyatwali, Mcharo na Guta na ujenzi wa miradi hiyo utakamilika ifikapo mwishoni mwa mwezi Mei, 2022. Serikali itaendelea kutenga bajeti katika mwaka wa fedha 2022/2023 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji kwenye Kata za Kabasa, Sazira, Kunzugu na Wariku.