Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 54 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 468 2016-06-30

Name

Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. GOODLUCK A. MLINGA (K.n.y MHE. MARWA R. CHACHA) aliuliza:-
Kumekuwepo na vifo vyenye utata wa kisiasa lakini inapotokea mpinzani kupoteza maisha havipewi kipaumbele katika upelelezi na hatua zinazochukuliwa:-
Je, Serikali inatoa tamko gani juu ya hali hiyo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Marwa Ryoba Chacha, Mbunge wa Serengeti, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi Tanzania inathamini maisha ya raia wake wote bila kujali rangi, kabila, itikadi za kidini na itikadi za kichama. Jeshi la Polisi linafanya kazi kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu zilizopo ambapo katika utekelezaji wa majukumu yake hatua mbalimbali huchukuliwa ili kuhakikisha haki inatendeka.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi imekuwa ikichukua hatua stahiki za kisheria kwa kila aina ya mauaji yanayotokea kwa raia na endepo mazingira ya mauaji yatakuwa yanalihusu Jeshi la Polisi basi Tume huru huundwa ili kuchunguza na kutoa ushauri kwa mamlaka husika na hatua stahiki huchukuliwa dhidi ya wahusika hao.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutimiza wajibu wake wa kuwalinda wananchi wake pamoja na mali zao bila upendeleo wowote.