Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 5 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 46 2022-02-07

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza: -

(a) Je, ni lini Serikali itajenga air traffic control tower yenye urefu wa kutosha kumuwezesha muongoza ndege kuona miundombinu yote ya runway, taxiways na maegesho ya ndege katika Uwanja wa Ndege wa Mtwara?

(b) Je ni lini Serikali itajenga jengo la muda la abiria lenye ukubwa wa kutosha wingi wa abiria wanaoingia na kutoka katika uwanja huo?

(c) Je, ni lini parking shade ya mitambo ya zimamoto na uokoaji itajengwa katika eneo lililopangwa kwenye master plan?

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI Alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mhe. Anastazia James Wambura wa Viti Maalum lenye sehemu (a), (b) na (c) kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kiwanja cha Ndege cha Mtwara kilijengwa na kuanza kutoa huduma katika mwaka 1952/1953. Kutokana na kuongezeka kwa matumizi ya kiwanja hiki yanayotokana na kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi na kijamii katika Mikoa ya Kusini, Kiwanja hiki kilihitaji kufanyiwa maboresho makubwa. Serikali kupitia Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), iliandaa Mpango Kabambe (Master Plan) uliopendekeza kupanua kiwanja hiki kutoka daraja Code 3C kwenda Code 4E (kwa mujibu wa ICAO). Kiwanja kitakapokamilika, kitakuwa na uwezo wa kuhudumia ndege kubwa za ndani na nje ya nchi zenye ukubwa wa Boeing 787-8 (Dreamliner).

Mheshimiwa Spika, Uboreshaji wa Kiwanja hiki umegawanywa katika awamu mbili, ambapo kwa sasa ujenzi unaoendelea ni wa awamu ya kwanza unaohusisha baadhi ya kazi zikiwemo urefushaji wa njia ya kuruka na kutua ndege (runway), ujenzi wa maegesho mapya ya ndege (Apron) na barabara zake za maingilio (taxiway).

Mheshimiwa Spika, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa Ujenzi wa mnara wa kuongozea ndege (Air Traffic Control Tower), Jengo la abiria (Airport Terminal Building) na kivuli kwa ajili ya maegesho ya mitambo ya zimamoto (Fire Fighting Equipment Shade) vitajengwa katika awamu ya pili mara baada ya kumalizika kwa awamu ya kwanza.