Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 4 Water and Irrigation Wizara ya Maji 31 2022-02-04

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya mradi mkubwa wa maji toka Ziwa Tanganyika kwenda Mpanda Mjini ili kutatua tatizo la maji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Moshi Selemani Kakoso, Mbunge wa Mpanda Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, upatikanaji wa huduma ya maji katika mji wa Mpanda ni wastani wa asilimia 60. Katika kuboresha huduma ya maji katika mji huo, Serikali mwishoni mwa mwezi Februari, 2022 itaanza utekelezaji wa miradi ya Kanoge II na Shangala. Kazi zitakazotekelezwa ni ujenzi vidakio vya maji vitatu, kufunga pampu, kujenga nyumba ya mitambo (pump house), ujenzi wa tenki lenye ukubwa wa mita za ujazo 200 na mtandao wa kusafirisha maji umbali wa kilometa 28. Miradi hiyo ipo kwenye hatua za manunuzi na inatarajiwa kutekelezwa kwa muda miezi sita na kuongeza uzalishaji wa maji kutoka mita za ujazo 6,000 hadi kufikia 8,000 kwa siku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mpango wa muda mrefu, Serikali imefanya tathmini ya awali ya kutumia Ziwa Tanganyika kuwa chanzo kuu cha maji kwa Mji wa Mpanda na maeneo ya kandokando mwa ziwa hilo. Katika mwaka 2021/2022 Wizara itakamilisha usanifu wa miundombinu inayohitajika kwa ajili ya utekelezaji mwaka wa fedha 2022/2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Mji wa Mpanda ni miongoni mwa miji itakayonufaika na mradi wa miji 28 na wakandarasi wataanza kazi katika mwaka wa fedha 2021/2022. Miradi hiyo itasaidia kufikia malengo ya kisekta yaliyopo ya zaidi ya asilimia 85 vijijini na zaidi ya asilimia 95 mijini ifikapo mwaka 2025.