Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 4 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 30 2022-02-04

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: -

Je, Serikali imejipangaje kutoa elimu ya utunzaji mazingira kwa wakulima wa mbogamboga ikiwemo pamoja na hatua za kuchukua ili kulinda mazingira katika Bonde la Mto Msimbazi?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Ladislaus Kamoli, Mbunge wa Segerea kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imebaini uharibifu wa mazingira ya Mto Msimbazi unaofanywa na wananchi wanapofanya shughuli si za kilimo tu bali pia uchimbaji wa mchanga pamoja na umwagaji maji machafu kwenye Bonde la Mto Msimbazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia kifungu cha 57(1) cha Sheria ya Usimamizi wa Mazingira Na. 20 ya mwaka 2004, katika kuhakikisha kwamba wakulima wa mbogamboga pamoja na wadau wengine hawaharibu mazingira ya Mto Msimbazi, Ofisi ya Makamu wa Rais imeandaa programu maalum za kuelimisha na kuhamasisha wananchi juu ya matumizi ya mwongozo wa mita 60 kwa lengo la kunusuru mazingira ya vyanzo vya maji ikiwemo Mto Msimbazi.

Aidha, Ofisi ya Makamu wa Rasi kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) imeelimisha watendaji wa Halmashauri zote za Mkoa wa Dar es Salaam kwa lengo la kuhamasisha wananchi wanaofanya shughuli za kimaendeleo kwenye Bonde la Mto Msimbazi kuzingatia kanuni na miongozo ya hifadhi ya mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile, Ofisi ya Makamu wa Rais kupitia mabalozi wa mazingira imeanza utekelezaji wa kampeni kabambe ya hifadhi na usafi wa mazingira ambapo suala la hifadhi ya vyanzo vya maji ni moja ya eneo la kipaumbele katika utekelezaji wa kampeni hiyo. Nakushukuru.