Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 3 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 24 2022-02-03

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuingiza lugha ya alama kwenye mitaala ya elimu nchini?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu Swali la Mheshimiwa Stella Alex Ikupa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa Lugha ya Alama katika kuondoa kikwazo cha mawasiliano kati ya wenye uziwi na wale wasio na uziwi. Katika kufikia lengo la kuingiza Lugha ya Alama kwenye Mitaala ya Elimu nchini, Serikali imekamilisha usanifishaji Kamusi ya Lugha ya Alama ya Tanzania ya mwaka 2020 na kurahisiha ufundishaji na ujifunzaji pamoja na mawasiliano. Vilevile, Serikali imekamilisha uandaaji wa Mwongozo wa Utekelezaji wa Mtaala wa Elimu ya Sekondari kwa wanafunzi viziwi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kuandaa walimu wenye taaluma ya Elimu Maalum katika fani ya Uziwi na Lugha ya Alama kila mwaka. Aidha, Serikali inaendelea kupokea maoni ya wadau kuhusu uboreshaji wa mitaala ya elimu na mafunzo nchini ambapo suala la matumizi ya Lugha ya Alama katika mitaala hii litazingatiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)