Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 3 Water and Irrigation Wizara ya Maji 22 2022-02-03

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya maji katika Jimbo la Momba?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Condester Michael Sichalwe, Mbunge wa Jimbo la Momba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, jukumu la Serikali ni kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma ya maji safi, salama na ya kutosha. Upatikanaji wa huduma ya maji Wilayani Momba ni wastani wa asilimia 59.07 kupitia visima vifupi (16), visima virefu (43), skimu za usambazaji maji (17) na matanki ya kuvunia maji ya mvua (3). Katika kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji Wilayani Momba, Serikali inatekeleza miradi ya maji katika Vijiji 13 vya Nkangamo, Itelefya, Mbao, Mkonga, Papa, Masanyinta, Kasamu, Samang’ombe, Lwatwe, Ivuma, Kapele, Mkutano na Kalungu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi zinazofanyika ni pamoja na ujenzi wa matanki saba (7) yenye ujumla ya ujazo wa lita 600,000, ulazaji wa bomba kuu umbali wa kilomita 32, vituo vya kuchotea maji 66 na ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji umbali wa kilomita 72. Utekelezaji wa miradi hiyo umefikia wastani wa asilimia 30 na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2022. Kukamilika kwa miradi hiyo kutaboresha upatikanaji wa huduma ya maji. Serikali itaendelea kutenga fedha za utekelezaji wa miradi mwaka hadi mwaka ili kumaliza tatizo la maji katika Jimbo la Momba na kufikia lengo la asilimia 85 ifikapo mwaka, 2025.