Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 54 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 465 2016-06-30

Name

Lucy Simon Magereli

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ISSA A. MANGUNGU (K.n.y MHE. LUCY SIMON MAGERELI) aliuliza:-
Machimbo ya Madini ya ujenzi yaliyoko Kigamboni yanatoa malighafi muhimu sana inayosaidia ujenzi katika jiji la Dar es Salaam; machimbo haya yanatoa ajira kwa zaidi ya wakazi 6,000 na ndiyo machimbo yenye mwamba laini kwa Mkoa wa Dar es Salaam ukilinganishwa na madini yanayotoka Goba:-
(a) Je Serikali haioni kuwa utaratibu wa kuratibu zoezi la kufunga machimbo haya utakosesha ajira kwa watu zaidi ya 6,000?
(b) Je, kwa kufunga machimbo hayo, Serikali haioni kuwa inawanyima fursa wananchi wa Dar es Salaam na Pwani kupata madini ya bei nzuri na kuwapunguzia gharama za ujenzi?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Lucy Simon Magereli, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, shughuli za utafutaji na uchimbaji wa madini hapa nchini hufanyika kwa mujibu wa Sheria ya Madini ya mwaka 2010. Sheria hiyo imeweka utaratibu Maalum wa uchimbaji wa madini ikiwemo kuacha umbali wa mita 200 kutoka makazi ya watu yaani bufferzone.
Umbali huo umekadiriwa kitaalam kuzuia madhara yanayoweza kutokea kutokana na shughuli za uchimbaji hasa maeneo ya makazi. Kwa sababu hizo sasa, Wizara ya Nishati na Madini inafanya mipango wa kutathmini namna bora ya kuendelea uchimbaji madini ya ujenzi katika mkoa wa Dar es Salaam hasa bila kuathiri mazingira, afya pamoja na maeneo ya wakazi kama nilivyoeleza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaona umuhimu sasa wa kupanua fursa na kuwezesha wananchi wengi kushiriki katika shughuli za uchimbaji wa madini haya. Hata hivyo Serikali inachukua fursa hii kutoa wito kwa Mheshimiwa Mbunge na wananchi wote kwa wachimbaji wote ili kuzingatia sheria zilizowekwa kwa mujibu wa sheria na kuongeza pato la Taifa.