Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 14 2022-02-02

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Primary Question

MHE. LUHAGA J. MPINA Aliuliza: -

(a) Je, ni sababu gani zilizopelekea kuchelewa kukamilika kwa ujenzi wa Bwawa la kufua umeme wa maji la Julius Nyerere?

(b) Je, kwa nini Mkandarasi ameshindwa kujaza maji kwenye Bwawa kufikia tarehe 15 Novemba, 2021 kama ilivyokuwa imekubalika?

(c) Je, ni hatua gani zimechukuliwa kutokana na ucheleweshwaji huo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama walivyosema wenzangu, nami kabla ya kujibu swali nimshukuru sana Mwenyekiti Mungu kwa afya na amani, lakini pia nimshukuru Rais, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuniamini kuhudumu katika nafasi hii ya Naibu Waziri wa Nishati. Pia niwapongeze Waheshimiwa Wabunge wenzangu wote kwa uchaguzi mkubwa, wa maajabu na wa furaha tulioufanya jana hapa Bungeni wa kumchagua Mheshimiwa Spika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa niaba ya Waziri wa Nishati naomba kujibu swali la Mheshimiwa Luhaga Joelson Mpina, Mbunge wa Kisesa lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo: -

(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, muda wa kukamilika kwa mradi kimkataba ni tarehe 14 Juni, 2022. Tarehe hiyo bado haijafikiwa.

(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, ili bwawa la Mwalimu Julius Nyerere lianze kujazwa maji, ni sharti liwe limejengwa kufikia kimo cha mita 95 juu ya usawa wa bahari ambapo kazi hiyo imekamilika. Aidha, ilitakiwa handaki lililojengwa kuchepusha maji ya Mto Rufiji kuzibwa. Kazi ya kuziba au kufunika handaki kwa kutumia vyuma maalum vizito ilihitaji mfumo maalum ambao ni wa kudumu wa mitambo ya kubebea milango hiyo (Hoist Crane system) kuwepo katika eneo la mradi. Mfumo huo unatengenezwa mahsusi kwa ajili ya kazi hii na kazi hii inapoisha crane hizo huondolewa na hazitumiki kwa kazi nyingine. Mitambo hiyo ilichelewa kufika kwa wakati kutokana na viwanda kufungwa na safari za meli kuathiriwa kutokana na UVIKO 19. Milango na mtambo wa kubebea tayari imefika na kazi za kuifunga zinatarajiwa kukamilika mwezi Machi, 2022.

(c) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wizara ya Nishati na TANESCO inaendelea kumsimamia mkandarasi aongeze kasi ya utekelezaji wa ujenzi ili kufidia muda uliopotea kwa kuongeza wafanyakazi na muda wa kazi.