Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 2 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 7 2022-02-02

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza upembuzi yakinifu wa ujenzi wa kiwango cha lami barabara ya Manyoni East – Heka – Isseke - Sanza hadi Dodoma?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GEOFREY G. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Manyoni Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Manyoni East – Heka – Isseke – Sanza – Chali – Igongo hadi Bihawana Junction Dodoma ni barabara ya Mkoa inayohudumiwa na Wakala wa Barabara (TANROADS). Barabara hii ina urefu wa kilometa 193 na kati ya hizo kilometa 124 ziko Mkoa wa Singida na kilometa 69 ziko Mkoa wa Dodoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua umuhimu wa barabara hii, Serikali imekamilisha usanifu wa kina na maandalizi ya nyaraka za zabuni kwa daraja la Sanza lenye urefu wa mita 75 lililopo kwenye barabara hii. Kazi hii ilikamilika mwaka 2018. Kwa sasa Serikali inatafuta fedha za kulijenga. Kazi za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa barabara hii zitafuata kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali kupitia Wakala wa Barabara (TANROADS) inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara hii ili kuhakikisha kuwa inaimarika na kupitika majira yote ya mwaka. Katika mwaka huu wa fedha wa 2021/2022, jumla ya Shilingi milioni 1,513.284 zimetengwa kwa ajili ya matengenezo mbalimbali ya barabara hii. Ahsante. (Makofi)