Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 2 Water and Irrigation Wizara ya Maji 5 2022-02-02

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JERRY W. SILAA K.n.y. MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawapatia maji wananchi wa Vijiji vya Kata za Imasela, Ilola, Lyamidati, Lyabukande na Nyida ambao wapo ndani ya Kilometa 12 kutoka katika mtandao wa maji ya Ziwa Victoria?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christina Christopher Mnzava, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, upatikanaji wa huduma ya maji katika Kata za Imasela, Ilola, Lyamidati, Lyabukande na Nyida zenye jumla ya vijiji 21 ni wastani wa asilimia 49.8.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha kuwa Vijiji vya Kata za Imasela, Ilola, Lyamidati, Lyabukande na Nyida vilivyopo ndani ya Kilometa 12 vinapata huduma ya maji kutoka katika mtandao wa maji ya Ziwa Victoria, Serikali imepanga kupeleka maji Kata ya Imasela kupitia awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mradi wa Tinde - Shelui. Utekelezaji wa mradi huo, ulianza mwezi Agosti, 2021 na kwa sasa, umefikia asilimia 15. Natarajia kuwa ifikapo mwezi Agosti, 2022 mradi utakuwa umekamilika.

Aidha, Serikali imepanga kufanya usanifu wa mradi wa maji wa Kata za Ilola, Nyida na Lyamidati ambao utaanza mwishoni mwa mwezi Februari, 2022 na kukamilika mwezi Juni, 2022. Ujenzi wa mradi huu unatarajiwa kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2022/2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Kata ya Lyabukande, usanifu umekamilika kwa ajili ya upanuzi wa mradi wa maji wa Ziwa Victoria katika vijiji vya Mwashagi na Buzinza. Ujenzi wa mradi katika Kijiji cha Mwashagi Kata ya Lyabukande utatekelezwa ndani ya mwaka huu wa fedha kwa kutumia fedha za UVIKO – 19, ambapo Mkataba wa ujenzi ulisainiwa tarehe 07 Januari, 2022 na unatarajiwa kukamilika kabla ya mwisho wa mwezi Juni,2022. Kwa upande wa Kijiji cha Buzinza, utekelezaji wa mradi utaingizwa katika bajeti ya 2022/2023.