Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 9 Water and Irrigation Wizara ya Maji 95 2021-11-12

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo la maji safi katika maeneo ya Ngara Mjini pamoja na maeneo ya jirani ya Murukulazo, Nyamiaga, Muruguanza na Buhororo yanayohudumiwa na Mamlaka ya Maji Safi Ngara?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Jimbo la Ngara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika Mji wa Ngara ni wastani wa asimilia 63. Uzalishaji wa maji ni mita za ujazo 1,500 kwa siku ambapo mahitaji ni mita za ujazo 2,500.

Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kuboresha huduma ya maji katika Mji wa Ngara, kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022, Serikali itachimba kisima kirefu chenye uwezo wa kuzalisha maji lita 80,000 kwa saa, kukarabati mtandao wa bomba umbali wa kilomita 1.73 na kuongeza mtandao wa mabomba ya kusambaza maji umbali wa kilomita 1.5. Kazi hizo zitaanza kutekelezwa mwezi Desemba, 2021 na kukamilika mwezi Aprili, 2022. Kukamilika kwa kazi hizo kutaboresha huduma ya maji katika Mji wa Ngara kufikia asilimia 78.9.

Mheshimiwa Spika, mpango wa muda mrefu ni kujenga mradi mkubwa wa maji utakaotumia chanzo cha Mto Ruvuvu. Mradi huo utanufaisha Mji wa Ngara na maeneo/Vijiji vya jirani vya Nterungwe, Nyakiziba, Kumutana, Mayenzi, Mukirehe, Murukulazo, Nyamiaga, Muruguanza na Buhororo. Kazi ya usanifu imepangwa kukamilika katika robo ya pili ya Mwaka wa Fedha 2021/2022. Mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa mradi anatarajiwa kupatikana kabla ya mwezi Julai, 2022.