Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 88 2021-11-11

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara yenye urefu wa kilometa 20 kutoka Nkome hadi Nzera?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Musukuma Joseph Kasheku, Mbunge wa Geita Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Nzera – Nkome ni sehemu ya Barabara ya Geita – Nzera hadi Nkome yenye urefu wa kilometa 54 inayounganisha Mji wa Geita ambayo ni Makao Makuu ya Mkoa na Miji Midogo ya Nzera, Nkome na Ziwa Victoria.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza kuandaa makabrasha kwa ajili ya kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina Barabara yote kutoka Geita – Nzera hadi Nkome (kilometa 54) kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetenga shilingi milioni 2,000 kwa ajili ya maandalizi ya kuanza ujenzi. Baada ya usanifu kukamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi.

Mheshimiwa Spika, wakati Serikali ikiendelea na maandalizi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara hii ili iweze kuendelea kupitika majira yote ya mwaka. Katika mwaka huu wa fedha 2021/2022 jumla ya shilingi milioni 1,162 zimetengwa kwa kazi hiyo. Ahsante.