Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 86 2021-11-11

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaipandisha hadhi barabara ya Igurubi – Mbutu – Igunga hadi Itumba yenye zaidi ya km 140 kuwa chini ya TANROADS ili ijengwe kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nicholaus George Ngassa, Mbunge wa Igunga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, taratibu za kupandisha hadhi barabara ni kwa mujibu wa Sheria ya Barabara Na. 13 ya Mwaka 2007 na Kanuni za Menejimenti ya Barabara za Mwaka 2009. Kwa vile suala hili ni la kisheria, ninamshauri Mheshimiwa Mbunge awasilishe maombi yake ya kupandisha hadhi Barabara ya Igurubi – Mbutu – Igunga – Itumba, yenye kilometa 102.8 kwenye Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Tabora. Bodi ya Barabara ya Mkoa itajadili maombi hayo na ikiridhia itawasilisha maombi kwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ambaye ndiye mwenye dhamana ya kupandisha hadhi ya barabara nchini. Ahsante.