Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 84 2021-11-11

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: -

Je, ni kwa nini Serikali haioni umuhimu wa kutenganisha Mahabusu/Magereza ya Watoto na Watu wazima ili kuwalinda Watoto dhidi ya vitendo vya ukatili wa kingono vinavyoweza kujitokeza?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nusrat Shaaban Hanje, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kulinda haki ya mtoto, Serikali ilitunga Sheria ya Mtoto Na. 21 ya Mwaka 2009 ambayo inakataza kifungo kwa watoto na kuweka mahabusu magerezani na iwapo italazimu kuwekwa mahabusu sharti awe chini ya uangalizi wa Kamishna wa Ustawi wa Jamii au mahabusu za nyumbani au chini ya uangalizi wa taasisi yeyote itakayotamkwa katika amri ya Mahakama.

Mheshimiwa Spika, Kanuni za Kudumu za Jeshi la Magereza za Mwaka 2003 Toleo la 4, chini ya Kanuni 488 zimeweka utaratibu mzuri wa kuwatenga wafungwa na mahabusu katika sehemu maalum na vyumba maalum kwa kuzingatia umri ambapo wafungwa na mahabusu watoto hutengwa katika mabweni yao maalum pasipo kuchanganywa na wakubwa.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, Serikali inalo Gereza la Wami ambalo ni maalum kwa watoto ama vijana waliokatika ukinzani wa sheria na kuhukumiwa vifungo ambavyo huhamishiwa huko na kutumikia vifungo vyao wakiwa peke yao kama vijana bila ya kufungwa na watu wazima.

Mheshimiwa Spika, aidha Serikali inaendelea kuwalinda watoto dhidi ya ukatili wa kingono na ukatili mwingine na kusimamia ipasavyo Sheria ya Watoto na Sheria zingine nchini zinazotoa ulinzi kwa watoto. Nakushukuru. (Makofi)