Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 8 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu 79 2021-11-11

Name

Latifa Khamis Juwakali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA K.n.y. MHE. LATIFA K. JUAKALI aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwahamasisha Vijana kushiriki katika shughuli za uzalishaji mali?

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, WENYE ULEMAVU (MHE. UMMY H. NDERIANANGA) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Latifa Khamis Juakali, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea na mikakati mbalimbali ya kuboresha mazingira yatakayoleta tija kwa vijana na kuwahamasisha kushiriki katika shughuli za uzalishaji mali. Mikakati hiyo ni pamoja na ifuatayo:-

(i) Kutoa mikopo yenye riba nafuu kupitia Mfuko wa Maendeleo ya vijana, ambapo hadi kufikia Oktoba, 2021 jumla ya vikundi vya vijana 957 vimewezeshwa kupata mikopo yenye thamani ya Shilingi Bilioni 6.7 ambayo imechochea ufanyaji wa shughuli mbalimbali za kiuchumi;

(ii) Kutoa mikopo isiyo na riba kupitia asilimia nne ya mapato ya ndani ya Halmashauri, ambapo hadi kufikia Juni, 2021 zaidi ya vikundi vya vijana 15,349 vimewezeshwa kupata mikopo yenye thamani ya Shillingi Bilioni 54.7;

(iii) Tumeendelea kutenga maeneo kwa ajili ya shughuli za uzalishaji mali, ambapo hadi sasa Halmashauri 111 zimetenga maeneo yenye ukubwa wa ekari 217,802 ambayo yamewanufaisha vijana 3,232; na

(iv) Tunaendelea kuendesha programu za mafunzo katika fani mbalimbali ikiwemo za ukuzaji ujuzi, Uanagenzi, Urasimishaji ujuzi pamoja na mafunzo ya kilimo cha kisasa. Kupitia mafunzo hayo, vijana 43,881 wamepatiwa mafunzo ya uanagenzi, Vijana 20,334 wamepata mafunzo ya kurasimisha ujuzi na Vijana 12,580 wamewezeshwa kupata mafunzo ya kilimo cha kisasa kupitia teknolojia ya kitalu nyumba.

Mheshimiwa Spika, kutokana na mikakati hii vijana wameweza kujipatia ajira pamoja na kujikita kwenye miradi ya uzalishaji mali ambayo imeendelea kuchangia ukuaji wa uchumi.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.