Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 7 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 78 2021-11-10

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza: -

Je, ni lini tatizo la upungufu wa mabehewa ya abiria na mizigo litatatuliwa katika Kituo cha Mpanda?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali Mheshimiwa Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Mpanda Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Shirika la Reli Tanzania (TRC) linakabiliwa na uhaba wa mabehewa ya abiria na mizigo. Ili kuondokana na changamoto ya upungufu wa mabehewa katika kituo cha Mpanda na sehemu zingine, Shirika linaendelea na ukarabati wa mabehewa na tayari limesaini mkataba wa ununuzi wa vipuri kwa ajili ya ukarabati wa mabehewa 37 ya abiria na 600 ya mizigo. Aidha, mwezi Juni, 2021, Shirika limesaini mkataba wa ununuzi wa mabehewa mapya 22 ya abiria utakaotekelezwa kwa kipindi cha miezi 12 na katika bajeti ya mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi bilioni 18.8 kwa ajili ya ununuzi wa mabehewa mapya 100 ya mizigo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchukua fursa hii kumwomba Mheshimiwa Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Mpanda, pamoja na wananchi wa Mpanda, kuwa na subira wakati Serikali inaendelea na zoezi la ukarabati na ununuzi wa mabehewa ya abiria na mizigo. Ni matumaini yetu kuwa pindi mabehewa yatakapowasili nchini na ukarabati kukamilika, tatizo la uhaba wa mabehewa kwa sehemu kubwa litakuwa limepatiwa ufumbuzi. Ahsante.