Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 7 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 77 2021-11-10

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: -

Je, ni lini barabara ya kutoka Magu – Bukwimba hadi Ngudu itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami ili kuunganisha Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba na Makao Makuu ya Mkoa wa Mwanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Mageni Kasalali, Mbunge wa Sumve, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Magu – Bukwimba hadi Ngudu ni sehemu ya Barabara ya Magu – Bukwimba – Ngudu hadi Hungumalwa yenye urefu wa kilometa 71. Serikali imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii tangu mwaka 2019. Baada ya kukamilika kwa usanifu Serikali inaendelea kutafuta fedha za kuanza ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Serikali ikiendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara hii ili iendelee kupitika majira yote ya mwaka. Katika mwaka wa fedha 2021/2022, jumla ya Shilingi milioni 596.576 zimetengwa kwa ajili ya matengenezo mbalimbali. Ahsante.