Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 6 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 67 2021-11-09

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID I. RAMADHANI aliuliza: -

Barabara ya kutoka Singida kupitia Mji Mdogo wa Ilongero – Mtinko hadi Hydom ni muhimu kwa uchumi wa Mkoa wa Singida, Manyara na Simiyu.

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Ilongero – Mtinko hadi Hydom kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu Swali la Mheshimiwa Abeid Ighondo Ramadhani, Mbunge wa Singida kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami Barabara ya Ilongero – Mtinko hadi Hydom yenye urefu wa kilometa 93.3. Mkataba wa kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ulisainiwa mwezi Oktoba, 2021 na kazi inatarajiwa kukamilika mwezi Novemba, 2022. Mara baada ya kazi ya Usanifu kukamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi. Ahsante. (Makofi)