Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 6 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 66 2021-11-09

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Chuo cha VETA katika Wilaya ya Handeni?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Reuben Nhamanilo Kwagilwa, Mbunge wa Handeni Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na mpango wa kujenga Vyuo vya Ufundi Stadi ikiwa na lengo la kuwa na Chuo cha Ufundi Stadi katika kila ngazi ya Mkoa na Wilaya. Tangu mwaka wa fedha 2019/2020, Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imetenga zaidi ya shilingi bilioni 76 kwa ajili ya kujenga Vyuo vya Ufundi Stadi 33, ambapo vyuo 29 ni vya ngazi ya Wilaya na vyuo vinne ni vya ngazi ya Mkoa. Mpaka sasa vyuo hivyo viko katika hatua mbalimbali za ujenzi.

Mheshimiwa Spika, katika Wilaya ya Handeni kuna Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Handeni ambacho pia kinatoa mafunzo ya ufundi stadi. Katika chuo hiki Serikali ilifanya ukarabati na ujenzi wa miundombinu uliogharimu jumla ya shilingi milioni 599.6 na kwa sasa Chuo kinaendelea kutoa mafunzo ya ufundi stadi.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi hiki ambacho Serikali inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha VETA wilayani humo, nashauri wananchi wa Handeni kuendelea kutumia vyuo vilivyopo nchini, ikiwa ni pamoja na Chuo cha Maendeleo ya Wananchi wa Handeni. Nakushukuru sana. (Makofi)