Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 6 Finance and Planning Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji 61 2021-11-09

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: -

(a) Je, kwanini Serikali isihamishe Kambi za Jeshi la Wananchi (JWTZ) Zanzibar ambazo zipo katikati ya makazi ya watu kutokana na kasi ya maendeleo ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza? na

(b) Je, Serikali inachukua hatua gani za kumaliza mgogoro wa muda mrefu wa mpaka kati ya wakulima na JWTZ kambi ya Kisakasaka?

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda nitoe shukrani zangu za dhati kwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu. Kwa kuniteua kuwa Mbunge na hatimaye kuniteua kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Lakini pia na kwako kwa ushirikiano ambao nimekuwa nikiupata tangu niteuliwe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya hapo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ussi Salum Pondeza, Mbunge wa Chumbuni kama ifuatavyo: -

(a) Mheshimiwa Spika, Makambi na Vikosi vya Ulinzi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania yameundwa kwa Mamlaka ya Sheria ya Ulinzi wa Taifa Na. 24 ya Mwaka 1966, ambayo imefanyiwa marekebisho na Sheria Na. 192 ya Mwaka 2002. Makambi haya na Vikosi yamejengwa kimkakati kukabiliana na tishio lolote dhidi ya Nchi yetu. Maeneo haya ni muhimu sana kwa ulinzi na usalama.

(b) Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uwepo wa migogoro baina ya Jeshi na wananchi wa Vijiji vya Sheha za Kisakasaka, Mwangani, Kombani, Fuoni na Kondemaji. Kwa nyakati tofauti serikali imefanya jitihada za kutatua mgogoro huu. Hivi sasa Wizara yangu inatekeleza Mkakati maalum wa miaka mitatu wa kupunguza au kumaliza kabisa migogoro ya ardhi baina ya Jeshi na wananchi.

Mheshimiwa Spika, kulingana na Mpango huu, Wizara imepanga kufanya upimaji na uthamini katika maeneo haya niliyoyataja katika robo ya pili ya Mwaka wa Fedha 2021/ 2022 ambayo ni robo hii. Wizara inawaomba wananchi kuendelea kuwa na subira wakati Wizara ikiendelelea na utekelezaji wa Mkakati huu wa upimaji na uthamini wa maeneo yote ya Jeshi.

(c) Mheshimiwa Spika, naomba pia nitoe rai kwa wananchi wanaoishi jirani na maeneo ya Jeshi, kuacha kuvamia maeneo hayo kwani ni hatari kwa usalama wao, na ni vigumu kwa Jeshi kuhamisha makambi kwa kuwa makambi hayo yamejengwa kimkakati. Nawasilisha. (Makofi)