Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 50 2021-11-08

Name

Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Zahanati katika Kata ya Ng’ambo iliyopo Tabora Mjini?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Andrea Kainja Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya kukamilisha maboma ya zahanati kwa fedha kutoka Serikali kuu na fedha za makusanyo ya ndani ya Halmashauri. Katika mwaka wa fedha 2020/2021 Serikali imetoa fedha shilingi bilioni 27.75, kwa ajili ya kukamilisha maboma ya Zahanati 555. Ambapo Halmashauri ya Manispaa ya Tabora ilipokea fedha ya shilingi milioni 150, kwa ajili ya ukamilishaji wa Zahanati ya Ituru, Igosha na Igombe.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetenga fedha shilingi bilioni 35.15, kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya zahanati 758 nchi nzima. Ambapo Halmashauri ya Manispaa Tabora imetengewa shilingi milioni 100 kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya Zahanati ya Zaire na Zahanati ya Kapunze kila moja shilingi milioni 50. Aidha, kupitia mapato ya ndani Manispaa ya Tabora imetenga fedha shilingi milioni 100 kwa ajili ya kukamilisha zahanati ya Mtendeni na Zahanati ya Igambilo, kila moja kwa shilingi milioni 50.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya zahanati yaliyojengwa na wananchi kote nchini. Aidha, Halmashauri ya Manispaa ya Tabora inashauriwa kutenga fedha kutoka katika mapato ya ndani kwa ajili ya kuanza ujenzi wa zahanati katika Kata ya Ng’ambo ili kusogeza huduma kwa wananchi.