Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 4 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 47 2021-11-05

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itashughulikia urejeshwaji wa Fedha za Wananchi wa Jimbo la Mtwara Mjini ambao walijiunga na Pride kwa ajili ya kupata mkopo?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Seleman Mtenga, Mbunge wa Mtwara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama inavyokumbukwa kuwa kulikuwa na shauri mahakamani lililofunguliwa mwaka 2016 kuhusu umiliki wa Kampuni ya Pride; baada ya kukamilika kwa shauri hilo na kutolewa hukumu tarehe 11 Novemba, 2018 kuwa Kampuni ya Pride Tanzania ni mali ya Serikali, Serikali ilifanya tathmini ya hali ya kampuni na kufuatiwa kwa ukaguzi maalum uliofanywa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na kutambua kuwa mali na madeni ya Kampuni hiyo ambapo taarifa ilionesha kuwa Kampuni hiyo ina madeni makubwa kuliko mali zilizopo.

Mheshimiwa Spika, kufuatia taarifa hiyo, Wizara ya Fedha na Mipango imeielekeza Ofisi ya Msajili wa Hazina kusimamia ufilisi wa Kampuni hiyo kwa kufuata taratibu za ufilisi wa Makampuni. Hivyo, kwa sasa Kampuni ya Pride ipo katika hatua za ufilisi. Madai yote yanayohusu Kampuni hiyo yatashughulikiwa kwa kufuata taratibu za ufilisi.