Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 4 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 44 2021-11-05

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali italifuta shamba la Mwakinyumbi Estate lililotelekezwa kwa muda mrefu na kuwapa wananchi wa Hale na maeneo jirani ili waweze kufanya shughuli za kiuchumi?

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Timotheo Paul Mnzava, Mbunge wa Korogwe Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Shamba la Mwakinyumbi Estate lilimilikishwa kwa barua ya toleo yenye Kumb Na. TRKF/76/ 65/AOM kwa muda wa miaka 99 toka tarehe 1 Aprili, 1989 kwa matumizi ya kilimo. Mmiliki alipewa masharti ya umiliki kwa mujibu wa Sheria za Ardhi. Miongoni mwa masharti hayo ni uendelezaji wa shamba na ulipaji wa kodi ya pango la ardhi kila mwaka.

Mheshimiwa Spika, ukaguzi uliofanyika wa ndani umebaini kuwa shamba hilo limetelekezwa na hakuna uendelezaji wowote uliofanyika na kwa sasa shamba hilo linadaiwa kiasi cha shilingi milioni 174.73 ikiwa ni kodi pamoja na malimbikizo kwa muda wa miaka 17 kuanzia mwaka 2005 hadi mwaka huu 2021. Kutokana na hali hiyo, Serikali ilianza kuchukua hatua za kisheria za kubatilisha miliki ya shamba husika kwa kutuma ilani ya kusudio la ubatilisho wa milki kwa siku tisini (90). Mmiliki hakuwasilisha utetezi wowote juu ya ilani ya ubatilisho aliyotumiwa kufuatia uvunjaji wa masharti kama ilivyoainishwa katika barua yake ya toleo. Hivyo, Serikali kwa sasa inaendelea na hatua za ubatilisho hatua zilizobaki mimi naandika barua kwa Mheshimiwa Rais kumshauri shamba hilo afute.

Mheshimiwa Spika, naomba kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa, ufutaji wa mashamba yaliyotelekezwa nchini ni zoezi endelevu kwa mujibu wa sheria ikiwa na lengo la kulinda maslahi mapana ya Taifa, wananchi na wawekezaji. Hatua hii inapunguza migogoro ya matumizi ya ardhi ambayo imekuwa ikijitokeza katika maeneo mbalimbali nchini.